Al Shabaab wasadikiwa kufanya unyama Garissa University College

19.08pm:Majeruhi:
 
Baadhi ya majeruhi wa tukio la Chuo cha Garissa 







 
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya ametuma risala za rambi rambi kwa familia za wale waliouawa katika shambulizi la chuo kikuu cha Garissa kazkazini mashariki mwa Kenya.Kiongozi huyo vilevile amewahakikishia wakenya kwamba serikali yake imechukua hatua za kuwapeleka maafisa wa usalama katika eneo hilo.Amewataka wakenya kuwa watulivu wakatu huu ambapo maafisa wa usalama wanakabiliana na wapiganaji hao.


17.00pm:Waziri wa usalama Kenya:
Waziri wa maswala ya ndani nchini Kenya Joseph Nkaiserry amethibitisha kuwa watu 15 wameuawa huku wengine 53 wakijeruhiwa kufuatia shambulizi la alfajiri katika chuo kikuu cha Garissa nchini Kenya.miongoni mwa waliokfariki ni walinzi wawili wa mlango wa chuo hicho.Akizungumza kutoka Garissa Nkaiserry amesema kuwa oparesheni ya kuwasaka wahalifu hao itaendelea hadi mateka wote waokolewe.


16.50pm:Mshukiwa mkuu:
Serikali ya Kenya imemtaja Mohammed Kuno kama mshukiwa mkuu aliyepanga njama za shambulizi la chuo kikuu mjini Garissa.Katika taarifa kwa vyombo vya habari waziri wa usalama nchini Kenya Joseph Nkaiserry alitoa zawadi ya dola 53,000 kwa mtu yeyote atakayemkamata mshukiwa huyo ama kutoa habari zake.Kuno anajulikana kama 'Gama'adhere kwa jina maarufu.

No comments