Hawa jamaa hatari kwa magoli ya vichwa
TEKERO inadaiwa lilikuwa ni jina la mganga mmoja maarufu wa
zamani aliyewahi kutamba katika moja ya mikoa ya Tanzania. Jina hilo
alikuja kupewa mmoja wa mastraika mahiri kuwahi kutokea nchini, Abeid
Mziba.
Nyota huyo wa zamani kutoka Kigoma aliyetamba na
timu kadhaa kabla ya kutua Yanga. Aliichezea Taifa Stars kwa takriban
miaka 10. Alikuwa mkali aisee. Mkali wa mabao ya kichwa. Wapo waliokuwa
wakiamini alichanjia kichwa na kumfanya apigapo mpira ulikuwa ukienda
kwa kasi kama umepigwa kwa miguu.
Siyo kama hakuwahi kufunga mabao kwa miguu.
Alikuwa akifunga ila kwa nadra mno, kama lile la mwaka 1987 kwenye
Uwanja wa Majimaji alipoipa Yanga ubingwa wa Ligi Daraja la Kwanza (sasa
Ligi Kuu).
Mwenyewe aliwahi kudokeza kuwa, alibashiriwa
kufunga bao hilo la mguu wa kulia na kuizamisha Majimaji, lakini ni
baada ya kukosa mabao mengi ya wazi. Ilidaiwa siku hiyo alikuwa amebeba
nyota ya jaa ya Yanga katika mchezo huo wa Songea.
Kichwa chake kilithibitisha kuwa ni fundi wa
mipira ya vichwa. Kipindi akiwa kwenye chati ndipo kukaibuka viatu aina
ya raba vilivyotengenezwa na vitambaa vilivyopapatikiwa sana. Achana na
HD, kuna maalumu vilivyopewa jina la Mziba kwa sababu mwenyewe alipenda
kuvivaa enzi hizo.
Wapo pia waliovuka mipaka na kutania eti miguu ya
Mziba ilikuwa ni ya kutembelea tu na siyo ya kuchezea soka. Ingawa
ukweli ni kwamba alikuwa akifunga na kutoa pasi zilizozaa mabao kwa
miguu hiyo hiyo iliyobezwa.
Sasa kama ulikuwa ukidhani baada ya kuondoka Mziba
katika ulimwengu wa soka la uwanjani, ndiyo ingekuwa mwisho wa kuibuka
kwa wakali wengine wa mabao ya vichwa umekosea.
Orodha ya wakali wa mabao ya vichwa waliomfuata
Mziba ni ndefu, ikiwajumuisha kina Hamis Gaga ‘Gagarino’, Said Mwamba
‘Kizota’, Said Mrisho ‘Zico wa Kilosa’, Kitwana Manara ‘Popat’ na
wengineo.
Hata hivyo, hapa chini tumewataja baadhi ya wachezaji walionyesha umahiri wao wa kufunga mabao ya aina hiyo.
SAMATTA
Nyota huyo anayekipiga TP Mazembe, anatajwa kama
mmoja wa mafundi wa mipira ya vichwa. Samatta aliyeanza kufahamika
African Lyon kabla ya kupita Simba kwa muda na kutimka zake kula maisha
yake Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, amekuwa akifunga mabao mengi kwa
vichwa kuliko miguu yake, ingawa hata huko nako ni hatari.
Mfano mdogo ni katika msimu wa 2011-2012 wa Ligi
ya Mabingwa Afrika, akiwa na kikosi hicho cha TP Mazembe kilichovutiwa
naye baada ya kung’ara na Simba msimu mmoja nyuma yake, alicheza mechi
nane.
Post a Comment