Mrwanda afunguka yake ya moyoni.. Shabiki wa Yanga Soma hapa




STRAIKA wa Yanga, Danny Mrwanda, anakatiza kilometa kadhaa katika mitaa ya Bagamoyo ambako wameweka kambi akifanya mazoezi binafsi kuhakikisha anaendeleza kasi yake ya kufunga mabao na kumshawishi kocha wake, Hans Van Der Pluijm, awe anampanga kikosi cha kwanza kila mechi.
Mrwanda tayari ana mabao manne katika Ligi Kuu Bara msimu huu na yote aliyafunga alipokuwa Polisi Moro, tangu alipojiunga na Yanga katika usajili mdogo hajafunga bao hata moja huku akiingia na kutoka kikosi cha kwanza.
Yanga ipo kambini Bagamoyo ikijiandaa na mechi ya kesho ya dhidi ya Ruvu Shooting.
Mrwanda anayewania nafasi na Amissi Tambwe, Kpah Sherman, Hussein Javu na Jerry Tegete, alisema: “Ushindani wa namba umekuwa mkubwa, kwa mchezaji anayejitambua ni lazima apambane. Ninakimbia barabarani kila asubuhi ili niwe imara.”
Mabao yake manne yanamweka katika nafasi ya pili kwa ufungaji  nyuma ya Mrundi wa Azam FC, Didier Kavumbagu aliyefunga mara tano. Wengine wenye mabao manne ni Rama Salim (Coastal Union), Ame Ally (Mtibwa), Rashid Mandawa (Kagera Sugar) na Simon Msuva (Yanga).

No comments