Kilichomfanya Okwi kuzimia Dk 5 chagundulika.. Soma hapa
Straika wa Simba, Emmanuel Okwi akitolea nje ya uwanja kwa njia ya Machela baada ya kuumia na kuzimia kwa muda
BAO kali na la aina yake limefungwa jana Jumapili na straika wa Simba, Emmanuel Okwi dhidi ya Azam FC dakika ya 19 akiwa nje ya eneo la hatari sekunde chache baada ya kupokea pasi ndefu ya kuburuza ya beki Hassan Kessy.
Straika huyo ambaye awali alishaapa kuifunga Azam
jana, alifunga bao la maana akiwazidi ujanja mabeki wa Azam pamoja na
kipa wao Mwadini Ally.
Walidhani kwamba Okwi atapiga krosi kwa wenzake
lakini badala yake, alisogeza kidogo mpira mbele kisha akamchungulia
kipa Mwadini na kupiga mpira ulioenda moja kwa moja ukagonga kidogo
mwamba wa juu na kutumbukia langoni.
Azam ilitumia dakika 57 kuwaziba midomo Simba
baada ya kusawazisha kupitia kwa Kipre Tchetche. Azam ilionekana kutulia
na kutawala sehemu kubwa ya mchezo ingawa wachezaji vijana wa Simba nao
walionyesha juhudi na ufundi wa aina yake.
Nyuma ya tambo hizo za Simba, Yanga ilikuwa
inaomba muda wote Simba iendelee na sare kama ilivyokuwa kwenye mechi za
kwanza za msimu huu. Simba ilitulia na kucheza soka la uhakika na
kuizidi Azam ambayo ilimtumia straika Didier Kavumbagu kuongoza
mashambulizi,hata hivyo bao la Simba lilidumu hadi mapumziko.
Kipindi cha pili Simba, ilimtoa Elius Maguli na
kumuingiza Simon Sserunkuma na Azam iliwatoa Frank Domayo na Didier
Kavumbagu na nafasi zao zilichukuliwa na Khamis Mcha na John Bocco.
Mabadiliko hayo yaliisaidia Azam ambayo ndiyo
klabu binafsi tajiri zaidi Afrika Mashariki, ilipata bao dakika ya 57
lililofungwa na Kipre Tchetche aliyepokea pasi safi ya Mcha ambaye ni
tegemeo la Zanzibar Heroes.
Baada ya kuingia kwa bao hilo, timu zote zilicheza
kwa kushambuliana kwa zamu lakini Simba ilionekana bado ina tatizo la
washambuliaji kuchoka mapema kwani waliruhusu mashambulizi mengi na
kulazimika kumtoa Said Ndemla na kumuingiza Shaaban Kisiga aliyeimarisha
kiungo.
Dakika za mwisho baada ya kuingia Kisiga, Simba
ilizinduka na kulishambulia lango la Azam ikipata kona mfululizo ambazo
hata hivyo hazikuweza kuzaa bao, mbaya zaidi Okwi aliumia dakika ya 61
alipogongana na Aggrey Morris wa Azam akiwa katika harakati za kufunga
na nafasi yake ilichukuliwa na Awadh Juma.
Okwi alitolewa uwanjani na kuwahishwa katika
chumba cha huduma ya kwanza uwanjani hapo ambako alitibiwa na kuzinduka
baada ya dakika tano hata hivyo baadaye alikimbizwa hospitali ya
Muhimbili na mpaka tunakwenda mitamboni alikuwa akifanyiwa vipimo zaidi.
Kwa sare ya jana Jumapili, Azam imebaki kileleni
ikiwa na pointi 21 ikifuatiwa na Yanga yenye pointi 20. Akizungumzia
mchezo huo, Kocha wa Simba, Goran Kopunovic alisema; “Nimeridhika na
sare hii kwani Azam ni mabingwa watetezi pia ni timu kubwa kwa hiyo sare
si matokeo mabaya.”
Kwa upande wake, Kocha wa Azam, Joseph Omog
alisema; “Wachezaji wangu hawakuwa makini na nafasi tulizopata sasa
tunajipanga na mchezo ujao.”
Post a Comment