Kabadeni atoa onyo kwa Boban, Cannavaro na Bathez



KOCHA wa zamani wa Simba, Abdallah Kibadeni, amewatolea uvivu wachezaji wanaojipachika majina ya nyota wa Ulaya kwa kuwaambia waache tabia hiyo kwani ni aibu kwao kwani wengi wanafanya madudu uwanjani.
Kibadeni alisema anashangazwa na ulimbukeni unaofanywa na wachezaji hao kulewa sifa kwa kuitwa majina ya mastaa wa nje wakati viwango vyao haviendani na na vya mastaa hao jambo libalodhihirisha kuwa hawana mwelekeo wa kufika mbali.
“Inashangaza mchezaji kujiita Mario Balotelli (straika wa Liverpool), siku  akienda Ulaya ataitwa nani? Ni aibu kwa wachezaji wa Tanzania wabadilike,” alisema Kibadeni.
Alisema wakati yeye anaichezea Simba kulikuwepo na mshambuliaji  Sunday Manara aliyepewa jina la  ‘Computer’ kutokana na uwezo mkubwa aliokuwa nao wakati huo, huku yeye akijiita  ‘King’ yote yaliendana na kazi zao na si vinginevyo.
Wachezaji wanaotumia majina ya mastaa wa nje kuliko ya kwao ni Ally Mustapha ‘Barthez’ (Yanga) akifananishwa na kipa wa zamani wa Ufaransa, Fabian Barthez, beki Nadir Haroub ‘Cannavaro’ anayefananishwa na beki wa zamani wa Italia, Fabio Cannavaro na Haruna Moshi ‘Boban’ wa Friends Rangers anayefananishwa na Zvonimir Boban wa Croatia.
“Sisi tulikuwa tukifanya mazoezi hata saa saba za usiku ili tutishe uwanjani, si hawa,” alisema Kibadeni.

No comments