Hii ndio siri ya utajiri mkubwa wa Manchester United..
MAJANGA yote hayajaitikisa kifedha Manchester
United baada ya kutajwa kwamba inashika namba mbili kwenye orodha ya
klabu tajiri duniani.
Man United iliyotoka kwenye
msimu mbaya ulioshuhudia Kocha David Moyes akifutwa kazi na timu
kushindwa kufuzu Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kumaliza nafasi ya saba
kwenye ligi. Lakini bado imekamata namba mbili kwa klabu matajiri
katika orodha iliyotolewa na Deloitte.
Miamba hiyo ya Old Trafford
imewapiga kumbo Bayern Munich na Barcelona baada ya mapato yao kupanda
kutoka Pauni 363.2 milioni hadi Pauni 433.2 milioni.
Man United ilipata mapato mengi
katika msimu wa 2013-14 kuliko klabu nyingine yoyote ya Uingereza na
hivyo kuwa namba mbili nyuma ya Real Madrid.
Real Madrid, ambao ni mabingwa
wa Ulaya ndiyo klabu matajiri zaidi duniani kwa sasa baada ya kuvuna
Pauni 456.5 milioni . Manchester City ni ya pili kwa utajiri kwa klabu
za England, lakini duniani inashika namba sita nyuma ya Paris Saint
Germain.
Vinara wa Ligi Kuu England,
Chelsea inashika nafasi ya saba, Arsenal ipo namba nane na Liverpool
ikishika namba tisa na kuzipiku Juventus, Borussia Dortmund na AC Milan.
Klabu 10 matajiri duniani; Real
Madrid (Pauni 459.5m), Man United (Pauni 433.2m), Bayern Munich (Pauni
407.7m) na Barcelona (Pauni 405.2m).
Zinazofuata ni PSG (Pauni
396.5m), Man City (Pauni 346.5m), Chelsea (Pauni 324.4m), Arsenal (Pauni
300.5m), Liverpool (Pauni 255.8m) na Juventus (Pauni 233.6m).
Post a Comment