Demu amponza straika wa Msimbazi




MSHAMBULIAJI wa zamani wa Simba, Ally Shiboli,  ambaye kwa sasa anakipiga African Sport ya Tanga inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza, ameweka wazi sababu iliyomshusha kiwango alipokuwa na  Wekundu wa Msimbazi  akisema ni kuchanganywa na mwanamke aliyekuwa mchumba wake.
Akifafanua tukio hilo Shiboli, alisema alijikuta anatoka katika hali ya mchezo baada ya mchumba wake huyo aliyekuwa anamhudumia kila kitu kama mke, kumsaliti na kuchukuliwa na rafiki yake.
“Nakumbuka niliitwa kwenye kikosi cha Taifa Stars tulienda kucheza Msumbiji niliporudi nikakuta yule mwanamke kabadilika tabia na mimi nilikuwa nimewekeza kwake, ilinifanya niumie hadi nishindwe kufanya vema katika timu yangu,” alisema.
Lakini anazungumzia maisha yake kisoka ya sasa kuwa ameamua kuweka kando suala zima la wanawake badala yake yupo katika harakati za kusaka nafasi ya kurejea katika timu zinazocheza Ligi Kuu Bara.
“Baada ya maumivu yangu kuisha niliamua jambo moja, kwanza kuna magonjwa, pia lazima nijenge maisha yangu mwenyewe na kama ni mke nitampata tu yule anayejitambua kwa hiyo kwa sasa nimeelekeza nguvu zangu katika soka sitaki kabisa kusikia ujinga wa mademu,” alisema.

No comments