TAMBWE AANZA HIVI



 
STRAIKA namba moja wa Ligi Kuu Bara msimu uliopita, Amissi Tambwe, ameanza tizi kwa morali ya nguvu kwenye klabu hiyo na kumshtukia kocha anayesubiri barua yake ya kufutwa kazi, Marcio Maximo sambamba na Msaidizi wake, Leonardo Neiva.
Tambwe ambaye si chaguo la Maximo, alipiga tizi kwa mara nyingine jana Alhamisi kwenye Uwanja wa Loyola, Dar es Salaam huku akipata ushirikiano mkubwa kutoka kwa wachezaji wenzake ambao wanaamini kwamba anaweza kuiziba mdomo Simba kwa kutumbukiza idadi kubwa ya mabao kuliko yale 19 aliyotupia akiwa Msimbazi msimu uliopita.
Wachezaji hao, makocha pamoja na wachambuzi wa soka wanadai kwamba Simba itajuta kuiuzia Yanga silaha. Katika mazoezi hayo, Maximo ambaye alisimama pembeni alikuwa akimfuatilia kwa karibu zaidi Tambwe na kumtathmini na kumshika mkono baadaye ingawa hakutaka kumzungumzia kwa lolote, aligoma pia kuzungumzia  sakata lake.
Akizungumza na Mwanaspoti Tambwe ametamba kufumania nyavu na kutetea ufungaji bora wa Ligi kwa msimu pamoja na kuipa Yanga ubingwa ikiwa ni njia moja ya kuthibitisha ubora wake.
“Nina nafasi ya kufunga zaidi kuliko msimu uliopita kutokana na mfumo wanaotumia Yanga, lakini pia aina ya wachezaji waliopo Yanga. Ninajiamini na ninafuraha ya kujiunga na Yanga, Naamini nitaweza kufanya kazi kubwa kwa kuwa nimetambulika Yanga kwa kazi nzuri niliyokuwa nikiifanya Simba siku za nyuma,” alisema Mrundi huyo.
“Kipindi cha mwisho nikiwa Simba sikuwa na furaha, iwe kwenye ligi au hata kwenye mazoezi, lakini sasa najiona nina amani na nitaweza kufanya kazi kubwa, kwa kushirikiana na wenzangu ninataka kuhakikisha ninashinda Kiatu cha Dhahabu lakini pia kuhakikisha Yanga inachukua ubingwa.
“Naamini kwa mfumo na kasi walizonazo wachezaji wa Yanga, nitaweza kufunika kwenye ufungaji mabao. Mpaka sasa anayeongoza ana mabao manne, mimi nina bao moja hivyo sipati shida kupambana  na kupata mabao mengi na kuwapiku waliopo juu yangu.”
 straika huyo amewaomba mashabiki wa Simba wasimchukie kwa kucheza kwake Yanga kwa vile viongozi wa Simba ndio waliomfukuza.
Tambwe amejiunga na Yanga akitokea Msimbazi  baada ya kuachwa na klabu hiyo kwa kile kilichodaiwa kuwa ameshuka kiwango.
Mrwanda amsifu Tambwe
Danny Mrwanda amemwangalia Tambwe katika mazoezi yao namna anavyojituma na kutamka: “Nimemwangalia Tambwe katika mazoezi yetu  kwa siku hizi chache, jamaa yupo vizuri na  ameifanya safu ya ushambuliaji iwe na ushindani zaidi. Ana uwezo katika kufunga, anajituma na anajua anachokifanya,

No comments