Rekodi hizi kali zinasubiriwa kuvunjwa pambano la watani
PAMBANO la watani wa jadi wa soka nchini Simba na Yanga la Machi
8 mwaka huu, lilikuwa ni pambano la 79 kwa wapinzani hao katika Ligi
Kuu ya Tanzania katika muda wa miaka 50.
Katika mchezo huo uliochezwa kwenye Uwanja wa
Taifa, Dar es Salaam Simba iliibuka na ushindi wa bao 1-0. Bao
lililofungwa na Mganda Emmanuel Okwi na lilikuwa ni bao la 164 baina ya
timu hizo tangu zianze kukutana mwaka 1965 katika ligi hiyo maarufu kwa
sasa kama Ligi Kuu ya Vodacom (VPL).
Siyo kwamba timu hizo hazijawahi kukutana zaidi ya
mechi hizo la. Zimeshakutana kwenye mechi za Ligi Kuu ya Muungano
iliyoasisiwa mwaka 1982-2014. Pia, zimeshakutana kwenye Klabu Bingwa
Afrika Mashariki na Kati (sasa Kagame) na michuano ya Kombe la Tusker.
Wameshaumana kwenye michuano ya Kombe la AICC,
Hedex, Kombe la Mapinduzi, Ngao ya Hisani na hata katika mapambano ya
kirafiki kama ile iliyopigwa jijini Mwanza mwaka 2003 na Yanga
kuishindilia Simba mabao 3-0.
Kwa kifupi timu hizo zimeshaonyeshana sana kazi
katika mechi mbalimbali, lakini katika Ligi Kuu zimeshakutana mara 79 na
Yanga kushinda mechi 29 na kupoteza 23 na zilizosalia zilikuwa sare.
Katika mechi hizo 79 Yanga imefanikiwa kufunga jumla ya mabao 87, kumi zaidi ya watani zao Simba ambao wamefunga mabao 77.
Mechi hizo za watani zina vituko vingi
vinavyokumbukwa ikiwamo timu kususia mechi, tukio la mchezaji kuanguka
uwanjani na kuzimia, beki wa Yanga Rajab Rashid ‘Double R’ kuushika
mpira akidhani refa amepuliza kipyenga na kusababisha penati. Unajua
ilikuwa lini? Oktoba 20, 1990 na Hamis Gaga ‘Gagarino’ alipiga penalti
na kukosa na mwishowe Simba ikalala mabao 3-1.
Hata hivyo, kuna rekodi tatu zinasubiriwa kwa hamu
na mashabiki kuona vikivunjwa. Mfungaji Bora wa Muda wote, kipigo
kikubwa zaidi cha 6-0 na ‘hat trick’ ya mechi hizo za watani hasa katika
Ligi Kuu.
KINARA WA MABAO
Kati ya wachezaji wote waliowahi kufunga mabao
katika mechi za watani hao wa jadi, hakuna anayemfikia rekodi ya Omar
Hussein ‘Keegan’.
Mshambuliaji huyo nyota aliowahi kuzichyezea timu
zote mbili kwa nyakati tofauti, ndiye kinara wa kufunga mabao mengi
katika mechi hizo za watani.
Keegan kwa sasa ni kocha alifunga jumla ya mabao
sita ambayo hayajaweza kufikiwa na yeyote mpaka sasa licha ya kustaafu
soka kitambo kirefu. Keegan aliyafunga mabao hayo akiwa na Yanga
aliyoichezea kwa karibu miaka 10 kabla ya kuhamia Simba.
Next
Next
Post a Comment