REKODI: Bado mabao 23 Ronaldo avunje rekodi ya bernabeu
Mabao yake matano ya juzi dhidi ya Granada katika ushindi mnono wa mabao 9-1 wa Real yamefanya afikishe mabao 300 na hivyo kubakisha mabao 23 kumfikia mkongwe Raul Gonzalez ambaye anashikilia rekodi ya kufunga mabao mengi zaidi klabuni hapo akiwa na mabao 323 katika mechi 741
HISTORIA inakaribia kubadilika Santiago Bernabeu. Ni
mshikemshike. Cristiano Ronaldo anaisaka rekodi ya kuwa mfungaji bora wa
muda wote Real Madrid na sasa amebakiza mabao 23.
Mabao yake matano ya juzi dhidi ya Granada katika
ushindi mnono wa mabao 9-1 wa Real yamefanya afikishe mabao 300 na hivyo
kubakisha mabao 23 kumfikia mkongwe Raul Gonzalez ambaye anashikilia
rekodi ya kufunga mabao mengi zaidi klabuni hapo akiwa na mabao 323
katika mechi 741.
Ronaldo pia amebakisha mabao manane tu kufikia
rekodi ya mkongwe anayeheshimika zaidi klabuni hapo marehemu, Alfredo di
Stefano ambaye alifunga mabao 308 katika mechi 396.
Hata hivyo, inaonekana Ronaldo anaweza kuvunja
rekodi zao akiwa amecheza mechi chache zaidi ambapo mpaka sasa
ameichezea Real Madrid mechi 287 tu na kuna kila dalili msimu huu tu
anaweza kuvunja rekodi hizo.
Mshambuliaji wa kimataifa wa Ufaransa, Karim
Benzema alikiri baada ya pambano hilo dhidi ya Granada kwamba Ronaldo
alikuwa katika kiwango cha hali ya juu.
“Ronaldo ni mtu wa ajabu sana. siku zote anatafuta
mabao na jinsi ya kuisaidia timu. Anastahili kila alichopata katika
maisha yake ya soka,” alisema Benzema ambaye katika pambano hilo
alifunga mabao mawili.
“Ronaldo, Bale na mimi tupo katika fomu nzuri,
kama ilivyo siku zote. Tunaisaidia timu na wakati mwingine tunafunga na
wakati mwingine hatufungi, lakini tupo katika hali nzuri na tutaendelea
kuwa hivyo mpaka mwishoni mwa msimu,” aliongeza Mfaransa huyo.
Kwa upande wa Ronaldo mwenyewe, aliwapongeza
wachezaji wenzake kwa kumsaidia kufunga mabao hayo matano wakati huu
akiikaribia rekodi ya Raul ambaye aliondoka klabuni hapo mwaka 2010
baada ya kuichezea timu hiyo tangu mwaka 1994.
“Nafurahi nimefunga mabao matano kutokana na kazi
nzuri ya timu. Asanteni kwa sapoti yenu,” aliandika Ronaldo katika
mtandao wake binafsi wa mawasiliano wa Twitter.
Ushindi huo wa Real Madrid ulikuwa muhimu baada ya
kupoteza mechi tatu kati ya tano za mwisho za La Liga ikiwemo pambano
dhidi ya watani wao wa jadi katika soka la Hispania Barcelona
walilochapwa 2-1.
Hata hivyo, ushindi huo uliiwezesha Madrid kukaa
kileleni kwa muda tu baada ya juzi usiku, Barcelona kuichapa Celta Vigo
bao 1-0 ambalo liliiwezesha kuendelea kuongoza La Liga kwa tofauti ya
pointi
Post a Comment