Haruna Niyonzima amwagiwa sifa


 Kiungo wa Yanga, Haruna Niyonzima


KOCHA wa Yanga, Hans Van Pluijm, amesema kiungo wake Haruna Niyonzima ameonyesha mabadiliko makubwa msimu huu tofauti na msimu uliopita ambapo alikuwa akipoozesha mchezo mara nyingi.
Niyonzima alikosekana katika kikosi cha Pluijm kwa karibu mechi zote za mzunguko wa pili wa msimu uliopita baada ya kocha huyo kudai kuwa amekuwa akipoozesha mchezo hivyo kupendelea kumtumia Mrisho Ngassa katika nafasi yake, lakini msimu huu amekuwa hakosekani katika kikosi cha Mholanzi huyo.
Kocha huyo wa zamani wa Hearts of Ouk ya Ghana alisema Niyonzima amekuwa mchezaji muhimu katika kikosi chake kwa sasa kutokana na uwezo wake mkubwa wa kufuata mipira nyuma na kupandisha timu.
“Ni mchezaji wa kiwango cha juu, anajua kucheza na mpira na kutembea uwanja mzima, amekuwa na mchango mkubwa sana kwetu kwa sasa,” alisema Pluijm
“Ukiwa kocha unahitaji aina ya wachezaji kama yeye, ni mchezaji anayeweza kukupa kitu unachokihitaji kwa wakati wowote, anatengeneza nafasi nyingi kwa wenzake,” alisema Pluijm.

No comments