Yanga yaonyesha jeuri ya pesa
KLABU ya Yanga kupitia Mwenyekiti wake, Yusuf Manji imewasilisha pendekezo mbele ya marais wanaounda Umoja wa Afrika (AU) la kuanzisha mashindano maalumu ya kupambana na ugonjwa wa Ebola na akatoa Dola 500,000 (sawa na Sh 870 milioni) kwa kuanzia.
Fedha hiyo aliyotoa Manji inakaribiana na fedha
anayopewa bingwa wa Kombe la Shirikisho, mashindano ambayo Yanga
inashiriki mwaka huu ikianza na BDF XI ya Botswana Jijini Dar es Salaam.
Bingwa wa Shirikisho hupewa Dola 625,000 (Zaidi ya
Sh1 bilioni) huku mshindi wa pili akipata Dola 432,000 (Sh700 milioni
za Tanzania).
Yanga imetenga Sh160 milioni kwa ajili ya mechi
mbili dhidi ya BDF ambayo ni bajeti tofauti kabisa na hiyo ya Ebola
aliyotoa Manji.
Pendekezo hilo la Manji amelitoa Alhamisi ya
Januari 29 wiki iliyopita jijini Addis Ababa, Ethiopia kulikofanyika
mkutano huo ambao kwa nchi ya Tanzania uliwakilishwa na Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Kikwete huku Manji akiwa mmoja wa
wageni.
Akizungumza na Mwanaspoti, Katibu wa Yanga, Dk.
Jonas Tibohora, ambaye naye aliongozana na Manji alisema katika kikao
hicho cha 24 cha AU, Manji amewasilisha pendekezo hilo akitaka nchi 54
za Afrika kushiriki katika mashindano hayo mafupi kusaka fedha za
kupambana na ugonjwa huo hatari unaiosumbua Afrika Magharibi. Katika
mapendekezo ya Manji anapendekeza watakaoshiriki mashindano hayo wawe
mabingwa wawili wa juu wa kila nchi.
Tibohora alisema katika pendekezo hilo la Manji
ambalo nchi zote zililiafiki, Manji ametaka mashindano hayo kuchezwa kwa
kanda za nchi husika ambapo mechi hizo zitachezwa kwa mfumo wa nyumbani
na ugenini huku kila klabu ikitakiwa kuchangia kiasi cha dola 100,000
(Sh173 milioni ) kama kiingilio.
Alisema lengo la Manji ni kutaka kuona soka
linachangia katika mapambano ya ugonjwa huo ambapo jumla ya kiasi cha
dola 10.8 milioni zitaweza kupatikana huku Mwenyekiti huyo akitangulia
kutoa hizo dola 500,000 za kianzio.
“Kwa kuwa mechi hizo zitakuwa zikiendeshwa kwa
mfumo wa nyumbani na ugenini, Manji ameomba klabu itakayocheza nyumbani
itoe nusu ya mapato ya kwenye mechi husika iende katika mapambano hayo
hapo pia klabu zitanufaika na nusu ya mapato hayo lakini pia ushindani
huo utazinufaisha baadhi ya nchi.”
KATUMBI KUFURU
TAJIRI wa TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya
Congo, Moise Katumbi, amekuwa na aina ya kipekee ya uendeshaji wa timu
yake kwa kuwapa zawadi watu wanaompa furaha uwanjani kwa wakati wote.
Habari kutoka kwenye vyanzo vya kuaminika hapa
Lubumbashi zinaeleza kuwa mchezaji anayefunga bao moja katika mechi za
kimataifa hupewa zawadi ya dola 10,000 (Sh 18 milioni) na anayetoa pasi
ya bao hilo hupewa zawadi ya dola 5,000 (Sh 9 milioni)
Post a Comment