Jinsi Simba ilivyojipanga kutwaa ubingwa leo.. Soma hapa
KAMA mikwara ya nje ya uwanja ni ubingwa, basi Simba ni bingwa wa Kombe la Mapinduzi hata kabla ya fainali ya leo Jumanne usiku dhidi ya Mtibwa kwenye Uwanja wa Amaan hapa Unguja, Zanzibar.
Simba ambayo ina uzoefu na mechi zaidi za fainali
kuliko timu yoyote nchini, imebadilika ndani na nje ya uwanja baada ya
kufuzu hatua hiyo.
Tangu wikiendi iliyopita, viongozi wote wa juu wa
Simba pamoja na wajumbe wa kamati zake, wamehamia karibu na kambi ya
timu yao mjini hapa na kumekuwa na vikao vya mara kwa mara na wachezaji
pamoja na kocha katika kuhakikisha wanazima kiburi cha Mtibwa ambayo
katika siku za hivi karibuni imekuwa ikiitesa Simba kwenye michezo ya
ligi na ile ya kirafiki.
Simba wamepandwa na mzuka hasa baada ya Yanga na
Azam kung’olewa kwenye michuano hiyo ambayo waliokuwa mabingwa mtetezi
KCCA ya Uganda walitolewa hatua ya robo fainali.
Habari za ndani zinadai kwamba vigogo watatu wa
klabu hiyo wamevuka mipaka kwa kumpa kocha mpya, Goran Kopunovic kikosi
ambacho wanataka kianze jambo ambalo vibosile wengine wakiongozwa na
Rais Evans Aveva wamelikemea vikali na kumtaka kocha kutotoa ruhusa kwa
watu kuingilia kazi zake.
Mashabiki wa Simba wameanza kumwagika kwenye
viunga vya Zanzibar tangu juzi Jumapili jioni na jana Jumatatu bendera
za rangi nyekundu zilitawala maeneo mengi ya Unguja ingawa Mtibwa nao
walikuwa wajanja kwa kufanya mazoezi na programu zao sirini sana.
Mchezo huo utakaoanza saa 2:15 usiku,
utazikutanisha timu zenye historia tofauti katika michezo mbalimbali ya
fainali ambayo wameshinda mara 15 wakipoteza mara 7.
Wekundu hao wamecheza fainali za Mapinduzi mara
nne na kuchukua mara mbili wakizifunga Mtibwa mwaka 2008 na 2011
wakiwafunga Yanga 2-0 huku wakipoteza dhidi ya Azam kwa mabao 2-1 mwaka
2012 na mwaka jana Mnyama alichapwa na KCCA mabao 2-0.
Mbali na mashindano hayo makali ya Simba katika
mechi za fainali pia yalionekana katika Kombe la Kagame ambalo
walichukua mara 6 ambazo ni nyingi kuliko klabu yoyote ya Tanzania hata
Afrika Mashariki yote.
Rekodi za Simba kwenye fainali pia zinaonyesha
Simba ilichukua kombe katika mechi za Kombe la Nyerere miaka ya
1984,1995,2000. Mtibwa wameingia fainali ya mapinduzi mara mbili miaka
ya 2007 alifungwa na Yanga na 2008 ambapo walifungwa na Mnyama.
Mwaka 2009 ilichukua Kombe la Tusker dhidi ya URA
ya Uganda, pia Mtibwa ikalichukua tena kombe hilo mwaka 2010 kwa
kuifunga Ocean View, pia wamewahi kuingia fainali ya Kombe la ABC Bank
mara moja na kufungwa na Simba mabao 3-2.
Simba iliyoweka kambi katika eneo lao la Mbweni
Unguja na ikijifua katika Uwanja wa Chuo cha Ualimu Chukwani, itaingia
uwanjani ikiwa na kikosi tofauti na kile kilichokubali kipigo cha bao
1-0 dhidi ya Mtibwa katika mechi ya kwanza ya hatua ya makundi.
Post a Comment