MANCHESTER United inatajwa kwenye mpango wa kumsajili winga ghali duniani na supastaa wa Real Madrid, Gareth Bale.
Staa huyo wa Wales anahusishwa na uwezekano wa
kurejea Ligi Kuu England ikiwa ni kipindi kifupi kupita tangu
alipong’oka Tottenham Hotspur na kutua Santiago Bernabeu kwa uhamisho wa
Pauni 86 milioni katika kipindi cha majira ya joto mwaka 2013.
Wakati dirisha la usajili la mwezi huu likiendelea
kuwa wazi, mchezaji huyo anaripotiwa kutaka kujiunga na Man United
inayonolewa na Mdachi, Louis van Gaal. Timu hiyo ipo kwenye mipango ya
kuboresha kikosi chake ili kurejea kwenye ubora.
Bale anaweza kufungua milango na kurejea kwenye Ligi Kuu England kujiunga na Man United kwa kuzingatia sababu hizi.
Mashabiki wa Real Madrid hawamkubali
Licha ya kuwa na mwenendo mzuri na kiwango
kisichoshaka katika kutikisa nyavu huku mabao yake akiyafunga kwenye
mechi muhimu zikiwamo za fainali, Ligi ya Mabingwa Ulaya na Copa del Rey
mwaka jana, Bale bado ameshindwa kuwa kipenzi cha mashabiki wa timu
hiyo.
Hali hiyo ilizidi kuwa mbaya zaidi Jumamosi
iliyopita wakati mashabiki hao walipochukua uamuzi wa kumzomea Bale kisa
hakumpa pasi Cristiano Ronaldo, aliyekuwa kwenye nafasi nzuri ya
kufunga. Ilikuwa kwenye mechi yao dhidi ya Espanyol.
Umaarufu wa Ronaldo pale Bernabeu
Uhusiano wa Ronaldo na Bale ndani ya uwanja siku
zote umekuwa mzuri na wenye kuheshimiana. Lakini, staa huyo wa Ureno
Jumamosi iliyopita alifanya tukio ambalo limemsababishia Bale matatizo
makubwa na sasa anaonekana hafai kwa mashabiki wa timu hiyo.
Kwa umaarufu wake, Ronaldo alionyeshwa kikerwa na
ubinafsi wa Bale katika mechi ya La Liga dhidi ya Espanyol kitu ambacho
kiliungwa mkono na mashabiki wa timu hiyo. Licha ya kufunga mabao
muhimu, Bale anaendelea kufunikwa na kivuli cha Ronaldo na hata kama
hakufanya ubinafsi makusudi, lakini jambo hilo litaendelea kumfanya Bale
aonekane si kitu.
Uhamisho wa Angel di Maria
Kama ilivyofanywa na staa wa zamani wa Real
Madrid, Angel Di Maria alipoamua kujiunga na Man United mwaka jana jambo
hilo linaweza kumshawishi Bale akaamua kufuata nyayo zake.
Post a Comment