Lazima awaue tu.. Hii ndio Staili mpya ya Tambwe






MSHAMBULIAJI wa Yanga, Amissi Tambwe, sasa ni wa kufunga kwa staili yoyote baada ya juzi Jumapili kufunga bao lake la kwanza kwa mguu msimu huu lililoingia katika rekodi ya Afrika.
Tambwe ambaye alisajiliwa na Yanga akitokea Simba Desemba mwaka jana, kabla ya mechi ya jana tayari alikuwa ameifungia timu hiyo mabao matano katika mashindano ya Ligi Kuu Bara na Kombe la Shirikisho.
Katika mabao hayo ambayo matatu aliyafunga katika Ligi Kuu Bara na mawili katika mechi ya awali ya Kombe la Shirikisho, Mburundi huyo alikuwa ameyafunga yote kwa njia moja ya kichwa.
Wakati juzi akiifungia Yanga bao la tatu dhidi ya Platinum bao ambalo pia likiwa la tatu kwake katika michuano hiyo, alionyesha kubadilika akifunga kwa mguu wa kulia akimalizia kazi safi ya mshambuliaji Mrisho Ngassa.
Bao hilo limemfanya mshambuliaji huyo kufikisha mabao sita msimu huu na matano kati ya hayo akiyafunga kwa kichwa akifungana na Ngassa ambaye naye ana mabao matatu katika Kombe la Shirikisho.

No comments